Katika dunia ya leo yenye ongezeko la mashambulizi ya mtandao hatuwezi kuishi bila kinga ya virusi. Kinga ya virusi ni mfumo wa usalama wa mtandao wa maunzi ngumu au program tumizi iliyotengenezwa kukataza kuingia sehemu iliyozuiliwa ya mtandao. Katika hali ya kawaida, huduma ambazo hazitakiwi kufikiwa katika eneo dogo la mtandao zimelindwa kwa kinga ya virusi. Kuna aina mbali mbali nzuri za kinga ya virusi ya maunzingumu inayotumika sokoni, hata hivyo katika hali ambayo bei ni tatizo, vibadala nafuu kama pfSense vinaweza kutumika.
pfSense ni program tumizi kamili ya kukinga virusi inayotumika katika kompyuta binafsi kutoa huduma zote muhimu kama za vitumi vya kibiashara. pfSense ina msingi kwenye program tumizi rafiki ya FreeBSD ikiwa na seva za mtandao LightPD na PHP. Pia pfSense inaingiliana vizuri kimtandao na hivyo kurahisisha usimamizi wake.
Licha ya uwezo wake wa kukinga virusi, pfSense ina uwezo mkubwa na rahisi wa kufikia sehemu mbalimbali na inaweza pia kutumika kama mahali pa kufikia bila waya, kutumika kwenye VPN na vile vile kutumika kwenye Seva ya DHCP. pfSense inaweza kufanya kazi vizuri kwenye mtandao tata na kuweza kukinga mtandao wako kwa gharama ndogo.
TZ-CERT inakushauri kufikiria kutumia kinga ya pfSense kama mtandao wako hauna kinga ya virusi na gharama ni tatizo.
Licha ya pfSense kuna kinga za virusi nyingine za kufikiria. Baadhi ni smoothwall na Untangle NG.
Unaweza kujifunza zaidi kuhusu pfSense katika tovuti yao https://www.pfsense.org