Taarifa yoyote iliyochapishwa kwenye tovuti hii na Tanzania – CERT pamoja na mengine yakiwemo mapendekezo yaliyotolewa na Tanzania CERT kwa watumiaji katika kutatua matukio ya kiusalama wa kompyuta, yametolewa katika misingi ya ‘kama yalivyo.’
Makosa au kuachwa kwake kunaweza kutokea wakati wa kutayarisha taarifa zilizomo ndani ya tovuti hii .Kwa hiyo kabla ya kutegemea taarifa zilizochapishwa, mtumiaji ni lazima awe huru kuhakiki usahihi, ukamilifu na umuhimu kwa matumizi yao na kwamba ni taarifa za hivi karibuni.
Tanzania CERT haikuhakikishii aina yoyote ya matumizi ya taarifa zilizochapishwa kwa kuelezwa au kudhaniwa. Taarifa iliyochapishwa inatolewa kama taarifa ya jumla tu na kwa kuelewa kwamba Tanzania CERT haitoi ushauri wa kitaalamu kuhusu jambo mahususi.
Taarifa zilizochapishwa humu zinaweza kujumuisha maoni au mapendekezo ya chombo kingine na si lazima yawe ni maoni ya Tanzania CERT, au kuonyesha ahadi kwa hatua ya kuchukuliwa.
Kama una maswali yoyote kuhusu taarifa zilizochapishwa ndani ya tovuti ya Tanzania CERT tafadhali wasiliana nasi kupitia info@tzcert.go.tz